Saturday 20 August 2016

KILIMO BORA CHA KITUNGUU SAUMU

Kitunguu saumu ni moja kati ya zao bora lenye manufaa mengi kwa matumizi ya kila siku kwa maisha ya mwanadamu, kiafya, Kitabibu na kwaajili ya kutengeneza au kuchanganyia katika dawa tofauti. Pia ni kiungo mausui katika mambo ya mapishi.

Zipo aina tisa za kitunguu saumu ambazo hulimwa hapa duniani katika maeneo mbali mbali. Aina za kitunguu saumu maarufu kwa matumizi ya kawaida  ni tatu, ambazo ni;-

SOFT NECK---ni nyeupe huzaa kwa muda mfupi.

SILVER SKIN---vina rangi ya silver vikikaushwa vinauwezo wa kukaa hadi mwaka                                          mmoja.

ANTICHOKE---vina rangi nyekundu kwa mbali.
1.    Kitunguu saumu chenye mafuta makali
2.    Kitunguu saumu chenye madini ya protini
3.    Kitunguu saumu chenye madini , protini na mafuta mepesi.
Hiki ndicho tulacho kila siku hapa kwetu na wengi hutumia kama dawa wakati hakina sifa za kuwa dawa.

NAMNA YA KULIMA
Kitunguu hiki hulimwa maeneo yenye baridi, uwanda wa jua hafifu, mvua za wastani na joto hafifu, ardhi iwe nyeusi naa yenye rutuba na mfinyazi, kusiwe na upepo mkali au ukungu mwingi.
Hulimwa kwa kuandaa kitalu na kupandikizwa baada ya kufika urefu wa inchi 6-14, hupandwa kwa mstari na mche hadi mche ni nchi 3-4 na mstari kwa mstari ni nchi 12.
Kwa kifupi zao la kitunguu saumu ni gumu kulilima kwani hustawi katika maeneo machache sana hapa duniani . Kwa hapa Tanzania hustawi katika mkoa wa Manyara wilaya ya Mbulu, Hannang na Babati kidogo, Mkoa wa Kilimanjaro na kwa eneo lolote ambalo hali inaendana na maeneo tajwa hapo juu. Pia kwa Mkoa wa Morogoro vinalimwa maeneo ya Mgeta.

UANDAAJI WA SHAMBA

Tifua udongo kidogo kasha ufanye hallowing ili kurahisisha upandaji na ukaaji wa mimea tu. Tengeneza tatu za mita 1 hadi 1.5, upana mita 10 urefu. Kwa upande wa mbolea inashauriwa utumie WINNER.


UPANDIKIZAJI
Vibanguliwe na vipandwe kwa kuelekezea mizizi chini na kina cha wastani 2.5 inchi, mbolea ya samadi hushauriwa zaidi kutumika, huvunwa baada ya miezi 4-6 kulingana na hali ya hewa na aina ya hali ya mbegu iliyotumika.

SPACING/MUACHANO WA MBEGU NA MBEGU
Mstari hadi mstari ni inchi 8 na mmea hadi mmea ni inchi 6 yaani (8*6) inchi.

KIWANGO CHA MBEGU
Kiwango cha mbegu ni kilo 200-300 kwa heka moja.

MAVUNO
Mavuno ni tani 5 – 6 kwa heka moja.

UANDAAJI WA MBEGU
Kitunguu saumu hupandwa “BULB” na siyo mbegu kama vitunguu maji. Ni ile Punje ambayo imekuwa na kukomaa vizuri na isiyoathiriwa na magonjwa.

MAGONJWA
1.    Vitunguu saumu havishambuliwi na magonjwa kama ilivyo kwa mazao mengine.
2.    Mimea ikianza kutoa maua , yaache yawe marefu hadi yajikunje kisha utayakata ili kuongeza  uzalishaji.
Wadudu wasumbufu ni THRIPS na ukungu upande wa magonjwa.
Kwa upande wa ukungu anza na RIDOMILL GOLD upulizie mara nne kisha malizia na score kwaajili ya Thrips tumia ACTARA au MATCH.
Hushambuliwa na magonjwa kuanzia wiki ya tatu hadi ya saba, tumia madawa ya kupuliza yatumikayo kwa nyanya na vitunguu vya kawaida.

SOKO
Kwa Kariakoo kilo moja  ni kati ya shilingi 4000 – 6000. Ila kwa ujumla ni kati ya bidhaa ambayo inayohitajika kwa wingi ndani na nje ya nchi.
Tunakutakia kila lakheri katika safari yako ya Kilimo bora.

MAKALA HII IMEANDALIWA NA STANLEY NGOLE, MTAALAM WA MASUALA YA KILIMO.
Stanley Ngole,
+255 767 880 400,
shambani.kwetu.leo@gmail.com

No comments:

Post a Comment