Yafutayo ndiyo
mahitaji kwa ajili ya kutengenezea chili souce;
a) Pilipili mbuzi nyekundu
robo 1/4 kilo.
b) Nyanya kilo moja.
c) Kitunguu swaumu
kikubwa kimoja.
d) Mafuta ya kula
vijiko 7 vya chakula.
e) sukari vijiko
viwili vya chai.
f) maji ya moto
kikombe kimoja cha chai.
g) vinega vijiko 3 vya
chai.
Baada ya kuandaa
mahitaji hayo ya jinsi ya kutengeneza chili souce, twende kuona moja kwa moja
jinsi ya kutengeneza chili souce.
HATUA YA KWANZA.
-Kata Pilipili kuondoa
mbegu.
-menya nyanya kuondoa
mbegu pia.
-menya vitunguu swaumu
kisha vikatekate viwe
katika vipande vidogo vidogo.
NB; baada ya kumaliza
hatua hiyo ya maandalizi chukua Brenda, kisha saga mchanganyiko wote wa
malighafi ambazo nimezianisha kwenye hatua ya kwanza. Saga mchanganyiko huu
mpaka uone imetoka rojo laini.
HATUA YA PILI.
Ukishamaliza kusaga
mchanganyiko huu hapo juu jambo ambalo unatakiwa kulifanya ni;
*Chukua sufuria yenye
nafasi ya kutosha kwa ajili ya kupika mseto huu.
*Weka sufuria yako
jikoni, iache kwa sekunde kadhaa ili ipate moto pia kama kuna maji katika sufuria
yaweze kukauka.
*Baada ya kuona
sufuria yako imekwisha kupata moto, chukua mafuta ya kula yaweke kwenye
sufuria, yaache yachemke.
* mafuta yakichemka
chukua mseto wako mwagia katika sufuria yako, koroga mseto huo kuelekea upande
mmoja kwa dakika 30 huku mseto huo ukiendelea kuchemka.
* Baada ya dakika 30
epua mseto huo na uuache upoe, kisha funga katika vifungashio kwani mseto huo utakuwa
umeshakuwa chili souce.
Mpaka kufikia hapo
utakuwa umekwisha kutengeneza chili souce ambayo inafaa kwa ajili ya
matumizi ya binadamu kwani ni salama kwa ajili ya afya yetu.
No comments:
Post a Comment