![]() |
Mzinga wa Nyuki |
Ufugaji wa NYUKI unaweza kuwa chanzo
kizuri cha kipato kwa Wakulima.
Uzalishaji wa asali nchini Tanzania umekuwa ukitegemea sana
wafugaji wadogo wadogo, wanaotumia njia za kiasili kama vile mizinga ya magogo
au vyungu, kwa nyuki wa kiafrika ambao ni wengi sana kwenye mapori.
Ni muhimu kuwa na utaalamu wa kufuga nyuki.
Mkulima ambae anahitaji kufuga nyuki ni lazima awe na uelewa
wa mzunguko wa maisha ya nyuki. Anaye anza ni lazima aulize wafugaji wenzake
ambao wana uzoefu wa kutosha, au kujiunga katika kikundi cha ufugaji ili apate
ufahamu zaidi juu ya ufugaji wa nyuki.
Tafuta sehemu salama kwa
ajili ya mzinga
Ni vizuri kutafuta
mahali pazuri, salama, na penye sifa ya kufugia nyuki. Vifaa vyote
vikishapatikana jambo linalofuata ni kuchagua mahali gani pa kuweka mzinga. Ni
vizuri sehemu hii ikawa mahali ambapo makundi ya nyuki hukusanyika mara kwa
mara. Mara nyingine kupata eneo sahihi ni tatizo.
Ni vizuri kuzingatia yafuatayo:
ü
Kulingana na hali ya
kujilinda ya nyuki wa Afrika, haishauriwi kuweka mzinga shambani au karibu na
shamba (weka umbali wa mita 150-200
kutoka kwenye mazao au nyumbani)
ü
Mzinga ni lazima uwekwe
sehemu ambayo haitasababisha upotevu wa nyuki wanaporudi kutoka nje ya mzinga
(wasiingie kwenye kundi lisilokuwa lao)
ü
Mizinga isiwekwe
mbalimbali sana ili kuepusha usumbufu wa kutembea mbali kwa mfugaji wakati
anapokagua.
Eneo la kuweka mizinga ni lazima liwe :
ü
Kimya, mbali na jumuia
(hospitali, shule, na viwanja vya michezo) na maeneo ya biashara au viwanda.
ü
Karibu na maji
masafi-kandokando ya mto, mabwawa ya samaki, mabeseni ya maji au sehemu ya
matone.
ü
Iwe karibu na chakula
cha nyukimimea inayochanua, miparachichi,
ü
nazi, euculptus, migunga
n.k
ü
Iwe sehemu ambayo ni
kavu na isiwe sehemu ya tindiga kwani unyevu unyevu husababisha ugonjwa wa
ukungu (fungal disease) na pia huzuia utengenezaji mzuri wa asali.
ü
Iwe mbali na watu
waharibifu na iliyojificha kuepuka waharibifu.
ü
Sehemu ya mizinga ni
lazima iwe inafikika kirahisi kwa kipindi chote cha mwaka ili iwe rahisi
kuhamisha nyuki pale inapohitajika.
ü
Kuwe na kivuli cha
kutosha hasa wakati wa mchana jua linapokuwa kali, na kusiwe na upepo mkali.
ü
Iwe mbali na mashamba,
ambapo dawa za kuulia wadudu zinatumika.
ü
Vichaka au wigo
unaotenganisha mizinga na kuzuia wavamizi ni muhimu ili kupunguza ukali wa
nyuki.
Jinsi ya kuweka mzinga.
Baada ya sehemu ya
kuweka mizinga kupatikana, kinachofuata ni kuandaa mizinga kwa ajili ya kuweka
panapotakiwa.
ü
Safisha mzinga kuondoa
uchafu wote, utando wa buibui na aina nyingine za wadudu.
ü
Weka chambo kwenye
mzinga (wafugaji wa nyuki mara nyingi hutumia NTA) kwa kuipaka katika kuta za
mzinga kwa ndani.
ü
Mzinga unaweza
kutundikwa kwenye mti, kwenye nguzo, kuweka kwenye jukwaa au kwenye miamba. Hii
inategemea mkulima mwenyewe anapendelea njia ipi.
No comments:
Post a Comment